Majimaji kileleni
Majimaji imekwea kileleni mwa Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) baada ya kuilazimisha timu ya Lipuli sare ya bila kufungana siku ya Jumatano.
Sare hio imeifanya Majimaji kufikisha pointi nane na kuziacha timu za Friends Rangers, African Sports na Kurugenzi zenye pointi saba baada ya zote ukiondoa Friends Rangers kufikisha mechi nne.
Nayo, timu ya Kurugenzi Mufindi kutoka mkoa wa Iringa ilifanikiwa kuifunga African Lyon ya Dar es Salaam bao 1-0 kwenye uwanja wa Karume, jijini Dar.
Katika mchezo huo, Hassan Mkota aliipatia bao pekee na la ushindi timu yake y Kurugenzi katika dakika ya 66 kutokana na pasi ya kiungo Innocent Ndanje.
Post a Comment